Bembea: Maudhui ya Ndoa

Mwandishi amesawiri suala la ndoa kupitia wahusika wafuatao:

¾    Yona na Sara, Neema na Bunju na hata Asna. Kupitia ndoa za wahusika hawa masuala mengi ya mahusiano katika ndoa yanajadiliwa.

¾    Ndoa ya Yona na Sara inasawiriwa kama ndoa ya kizazi cha jana.Inaonyesha matarajio ya ndoa kulingana na jamii yao. Inaakisi malezi, majukumu ya mke na mume na matarajio ya wanajamii kuhusiana na watoto. Inachora picha ya majukumu kama yalivyopangwa na jamii ya Yona na Sara.

¾    Kulingana na jamii katika tamthilia ya Bembea ya Maisha, mwanamke anapoolewa anahitajika kuanzisha familia na mumewe. Anatarajiwa kujifungua watoto wa kike na vva kiume. Katika ndoa ya Yona na Sara, tunafahamishwa kuwa wanajamii waliwasema na kuwatafuna kama chingamu huku Yona akiitwa gumba na Sara kuitwa tasa. Hii ni baada ya kuoana na kukaa kwa muda mrefu bila kujaliwa na watoto (uk. 6). Ni wazi kwamba ndoa ya Yona na Sara imenyimwa hadhi katika jamii kwa kukosa mtoto wa kiume (uk. 7).

¾    Kulingana na kizazi cha jana, mke anatarajiwa kujifungua watoto wa kike na wa kiume na hasa wale wa kiume. Ndoa ya Yona na Sara inasutwa na kukejeliwa na wanajamii kwa kukosa mtoto wa kiume ambaye aliaminika angekuwa mrithi wa Yona (uk. 8). Wanajamii walimtaka Yona kumwoa mke ambaye angemzalia watoto wa kiume. Kulingana nao, Sara alikuwa ameshindwa kumzalia mtoto wa kiume. Unyanyapaa huu ulimsukuma Yona kuupokea ulevi na kuanza kumpiga Sara kipigo cha mbwa kwa kuwa hakumzalia mtoto wa kiume (uk. 9-10).

¾    Ni wazi kwamba ndoa ya Yona na Sara imenyimwa nafasi na hadhi katika jamii kwa kukosa mtoto wa kiume.

¾    Ndoa pia imesawiriwa kama kitu chema ingawa chenye changamoto zinazoweza kuvumiliwa. Sara anasema kuwa ndoa ni uvumilivu na wala Sio watoto na hakuna ndoa isiyokosa doa. Sara anaivumilia ndoa yake na Yona. Anavumilia kuchapwa, kudharauliwa na kudhulumiwa. Sara anamvumilia mumewe hata baada ya dhiki hizo. Fauka ya hayo yote, anamshauri Neema aivumilie ndoa yake na Bunju. Vilevile, anamshauri Asna kumtafuta mume aolewe (uk. 33, 67).

¾    Ndoa huakisi suala la malezi. Yona na Sara wanaonyesha malezi kwa kuwalea mabinti wao. Sara anawafurahia watoto wake na kujitahidi kuwalea ipasavyo.

¾    Ndoa ya Neema na Bunju ni ya kizazi cha leo. Neema na Bunju wamesoma, wamehitimu na wameajiriwa na kuanza familia yao. Wanashirikiana katika masuala ya matumizi ya pesa. Bunju anashughulikia majukumu ya familia yake na Neema. Amemruhusu

¾    Ndoa ya Neema na Bunju ni ya kizazi cha leo. Neema na Bunju wamesoma, wamehitimu na wameajiriwa na kuanza familia yao. Wanashirikiana katika masuala ya matumizi ya pesa. Bunju anashughulikia majukumu ya familia yake na Neema. Amemruhusu Neema kutumia mshahara wake kuwasaidia wazazi wake. Ndoa katika tamthilia hii imesawiriwa kama uhusiano unaofaa kuleta heshima na uvumilivu. Bunju anamlalamikia Neema kwa kukosa kujulishwa kuwa mama mkwe wake anarejea kijijini bila yeye kujulishwa. Suala hili linamkera sana Bunju na kumuona Neema kama mke asiye na heshima (uk. 48).

¾    Neema anasisitiza kuwa amempa mumewe heshima ya kutosha (uk. 49). Jambo la ndoa limesawiri majukumu ya mke na mume. Katika ndoa ya Bunju na Neema, mume ana majukumu ya kulipa karo, kulipa kodi ya nyumba na majukumu mengine. Jambo hili linaonyesha kuwa Bunju ni mume aliyewajibika. Kwa upande mwingine, Neema ana jukumu la kuwatunza wazazi wake.

¾    Katika ndoa ya Sara na Yona, Yona anasawiriwa kuwa na jukumu la kuwasomesha wanawe. Hata baada ya Sara kwenda mjini kwa ajili ya matibabu, Yona anachukua majukumu nyumbani kama vile kushughulikia mifugo na kuondoa mtama shambani. Katika mwisho wa tamthilia, Yona anamwahidi Sara kuwa atayachukua majukumu yote kama mumewe na atamshughulikia katika kila hali. Yona pia anaonyeshwa kuwa na jukumu la kumjuza Sara kuhusu mikutano ya vyama vya kina mama.

¾    Ndoa pia imesawiriwa kama jambo lililojaa bughudha. Kulingana na Asna, ndoa ina mateso na imejaa masharti mengi. Asna anaona ndoa ya dadake Neema imejawa na matatizo yasiyoweza kuvumilika. Anasema kuwa Bunju ni mchoyo na asiyetaka kumsaidia mtu (uk. 33, 45). Asna vilevile anaiona ndoa ya wazazi wake kama iliyojawa na mateso.

¾    Anamweleza mamake kuwa amedhoofishwa na mateso aliyoyapata katika ndoa yake (uk. 53). Hali hii inamfanya Asna kusawiriwa kama msichana anayetaka kuyajenga maisha yake bila mume.